Shirikisho la Kimataifa la Makanisa ya Kipentekoste Ulaya/Afrika
ni Ushirika wa Ulimwengu wa Kikristo wa Kitume ni muungano wa ulimwenguni pote unaoundwa na wale wanaoshikamana na mafundisho ya mtume kwa maneno na matendo. Maagizo ya ushirika huu yametolewa na maandiko yanayosisitiza umoja wa watu wa Mungu. Bwana wetu Yesu Kristo alifundisha hivi: “...ili wote wawe na umoja, kama yeye na Baba yake walivyokuwa umoja.
Mtume Paulo alitangaza kwamba “...tuwe na nia moja, nguvu moja, wala si mafarakano.
Historia ya Kanisa la Kipentekoste la mitume la karne ya 20, ingawa ni tukufu; kwa huzuni yaonyesha kwamba mabishano na mizozo mingi imeingia kati ya akina ndugu.
FIEPE/A inajaribu kubadili mwelekeo huu kwa kujitahidi kuondoa migawanyiko na vizuizi vilivyoachwa na wanadamu, kuleta mgawanyiko kwa Mwili wa Kristo na kuchanganyikiwa kwa ulimwengu! Neno la kinabii la Yesu, “Ulimwengu ujue ya kuwa umenituma” linaweza tu kutimizwa kwa umoja. Hakika si mgawanyiko.